BARCA YAENDELEZA DOZI, SUAREZ HAKAMATIKI

Luis Suarez sasa hakamatiki baada ya kukaa kileleni kwa ufungaji bora wa mabao katika La Liga.

Suarez sasa ana mabao 34 na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid ambaye ana mabao 31, hivyo kuamsha kasi ya ugombeaji wa tuzo ya mfungaji bora ya La Liga maarufu kama Pichichi.

Suarez ameifungia Barcelona mabao manne katika mechi ambayo Barcelona imeitwanga Sporting Gijon kwa mabao 6-0.

Kabla ya hapo, Barcelona ilishinda kwa mabao 8-0 dhidi ya Derpotivo la Coruna.

Hivyo kumfanya Suarez awe amefunga mabao nane katika mechi mbili.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment