TANZANIA YAPOROMOKA VIWANGO VYA FIFA




Tanzania imeporomoka kwa nafasi tano kwenye orodha ya viwango vya ubora wa soka duniani vilivyotolewa leo na Shirikisho la soka la kimataifa  FIFA.
Hiyo ina maana kwamba Tanzania sasa imeangukia katika nafasi ya 130 kwenye viwango hivyo.

Tanzania hawajahesabiwa mechi yoyote ya hivi karibuni ambapo Taifa Stars ilishinda bao 1-0 dhidi ya Chad katika mechi ya kwanza ugenini lakini Chad wakajiondoa na hawakushiriki mechi ya marudiano jijini Dar es Salaam. 

CAF ilifuta matokeo hayo dhidi ya Chad katika kundi G.

Miongoni mwa mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Uganda inaongoza ikiwa nafasi ya 72, Rwanda inafuata ikiwa nafasi ya 87, Kenya nambari 115, Burundi nambari 122 na Tanzania nambari 130 

Orodha ya mataifa tatu bora Afrika ni kama ifuatavyo:
Algeria
Ivory Coast
Ghana
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment