Samatta(kushoto) na Ulimwengu (kulia) |
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal
Malinzi amewatumia salamu za pongezi wachezaji Mbwana Samatta na Thomas
Ulimwengu wanaochezea klabu ya TP Mazembe ya Congo DR kufuatia kutwaa Ubingwa wa
Ligi ya Mabingwa Afrika jana kwa kuifunga timu ya USM Alger kwa jumla ya mabao
4-1.
Katika salamu zake kwenda kwa wachezaji hao, Malinzi
amewapa hongera kwa mafanikio waliyofikia ya kutwaa ubingwa huo wa vilabu
Afrika, na kuwataka waongeze bidii ili waweze kufanya vizuri pia katika
michuano ya Kombe la Dunia la Mabara litakalofanyika mwezi Disemba nchini
Japan.
Malinzi amesema kwa niaba ya familia ya mpira wa
miguu na Watanzania wote wanawashukuru kwa kuiwakilisha vizuri Tanzania
kimataifa, na sasa moyo huyo wa kujituma kwao waundeleleze katika mchezo dhidi
ya Algeria wikiendi hii kuwania kufuzu kwa fainali za kombe la Dunia 2018
nchini Urusi.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU NCHINI (TFF)
0 comments:
Post a Comment