Na Nicolaus Kilowoko
Mkuu wa kitengo cha habari na Mawasiliano cha klabu ya
Simba, Haji Manara kesho anatarajiwa kukwea pipa kwenda nchini India kwa ajili
ya matibabu ya macho.
Manara alipatwa na matatizo hayo hivi karibuni ambapo
jicho lake moja lilipoteza uwezo wa kuona na lingine likiwa linaona kwa kiasi
kidogo.
“Ninapenda niliweke sawa hili, Mimi sikuomba watu
wanichangie pesa za matibabu isipokuwa walioguswa na tatizo langu ndiyo
waliojitokeza na kunichangia.Ninawashukuru walionichangia. Manake nimeona
niwaeleweshe watu ili isije ikaonekana kwamba Haji anaomba msaada,”alisema
Manara.
Siku chache zilizopita baadhi ya wanachama wa Yanga
wakiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Habari wa Yanga, Jerry Muro, walikwenda
nyumbani kwake na kumkabidhi kiasi cha shilingi 1,055,000 ambacho
walichangishana kupitia makundi mbalimbali ya mitandao ya kijamii.
0 comments:
Post a Comment