YANGA YAANGUKIA KWA TP MAZEMBE

Hatimaye timu ya soka ya Yanga imejikuta ipo kundi moja na TP Mazembe ya Congo DR kufuatia droo iliyochezeshwa leo Mei 24,2016.

Awali Yanga ilikuwa ikiombea ipangwe kundi moja na waarabu tupu ili ilipe kisasi cha kuondoshwa kwenye Klabu Bingwa na Al Ahly ya Misri lakini hatimaye leo imejikuta ikiangukia kwa Mazembe ya Congo, Medeama ya Ghana na MO Bejaia ya Algeria.

Ikumbukwe kuwa Yanga imeingia hatua hiyo kwa kuitoa Esperanca ya Angola kwa jumla ya mabao 2-1.

KUNDI A
Mazembe
Mo bejaia
Yanga
Medeama

KUNDI B
Etoile
FUS rabat
Kawkab
Ahly tripoli
Mechi hizo za makundi zitaanza Juni 17 mwaka huu na washindi wawili wa kila kundi watatinga nusu fainali.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment