MASHABIKI LIVERPOOL WAMSONONESHA KLOPP

Mashabiki wa Liverpool wakitoka uwanjani kabla ya mchezo kumalizika hapo jana


















Baadhi ya mashabiki wa Liverpool jana walimuacha peke yake kocha wao Jurgen Klopp mara baada ya mlinzi wa Crystal Palace, Scot Danny kufunga goli la ushindi katika dakika ya 82 ya mchezo na kufanya matokeo kuwa 2-1.

Hicho ni kipigo cha kwanza kwa kocha Jurgen Klopp tangu atue Liverpool hivi karibuni kuchukua mikoba ya Brendan Rogders aliyetupiwa virago mwezi uliopita.

Akielezea tukio hilo mara baada ya mchezo, kocha huyo raia wa Ujerumani alisema amesikitishwa sana na kitendo hicho cha mashabiki kumkimbia na kumuacha peke yake wakati timu ikihangaika kurudisha bao, hali anayoisema kuwa alijihisi mpweke zaidi na kusikitishwa sana na tukio hilo.

Klopp amewataka mashabiki kuwa wavumilivu na kwamba haipendezi kutoka uwanjani kabla ya dakika ya mwisho kwani kwenye mpira lolote linaweza kutokea na kwamba ni vizuri kuisapoti timu hadi mwisho.

Aidha katika tukio jingine, Klopp alishuhudia kuumia vibaya kwa mlinzi wake wa kati Mamadou Sakho ambaye leo atafanyiwa scan kuona ni muda gani atakua nje ya uwanja.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment