AZAM FC SAFARINI KUWAFUATA 'WANA LIZOMBE'

Azam FC asubuhi ya leo imetua kwenye uwanja wa ndege wa Songwe jijini Mbeya na kupanda basi kwenda Songea kuwavaa wenyeji Majimaji katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Mchezo huo utachezwa Jumapili ya keshokutwa kwenye dimba la Majimaji Songea.

Azam ilitua Mbeya saa 3 asubuhi na kufuatwa na basi lao kwa ajili ya safari ya kwenda huko Songea.

Kwa kawaida basi la Azam hutangulia mapema sehemu husika na kisha hutumika kuwapokea wachezaji pindi watumiapo usafiri wa ndege hasa ikitokea kwamba mechi inachezwa mikoa ya mbali na Dar es salaam.

Zifuatazo ni picha mbalimbali zikionyesha jinsi Azam ilivyopokewa na basi lao jijini Mbeya asubuhi ya leo.

NB: PICHA WA HISANI YA UKURASA WA FACEBOOK WA AZAM FC



Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment