Naibu Waziri wa habari,Utamaduni,Wasanii na Michezo
Anastazia Wambura leo ameitembelea kambi ya timu ya Taifa ya soka la wanawake
Twiga Stars na kuahidi kutoa motisha ya shilingi laki tatu kwa kila mchezaji
endapo wataifunga Zimbabwe siku ya Machi 5 mwaka huu.
Mchezo huo wa kuania kufuzu kwa fainali za Mataifa
ya Afrika kwa wanawake kati ya Twiga na Zimbabwe utachezwa kuanzia saa 10 jioni
kwewnye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Wakati akizungumza na timu hiyo Naibu Waziri
Anastazia amehaidi kila mchezaji kupata shilingi 300,000 endapo watashinda
katika mchezo huo.
Amesema kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau wa
michezo wamekusanya shilingi milioni 15 ambazo zitatumika kama motisha kwa
wachezaji hao.
Waziri Anastazia amesema ni kweli timu hiyo haina
wadhamini lakini wao kama Serikali wamepokea fedha hizo kutoka kwa wadau mbalimbali
wa soka na watazigawa kwa wachezaji hao endapo wataifunga timu hiyo katika
mchezo wao wa kwanza na katika mchezo wao wa marudiano utakaochezwa nchini
Zimbabwe.
0 comments:
Post a Comment