BINSLUM TYRE WANOGEWA NA MBEYA CITY FC




KAMPUNI ya Binslum Tyre ya jijini Dar es Salaam, leo imesaini mkataba wa miaka miwili  wenye thamani ya shilingi milioni 360 wa kuendelea  kuidhamini Mbeya City FC.

Mara baada ya kusaini mkataba huo, kaimu mkurugenzi wa kampuni hiyo Mohamed Binslum  alisema licha ya City kuwa na matokeo yasiyoridhishwa msimu uliopita lakini walilidhishwa kwa kiasi kikubwa namna ambavyo timu hii ilishiriki katika kuitangaza bidhaa yao  na kuifikisha sehemu ilipostahili kusfika.

“City haikuwa na matokeo mazuri msimu ulipopita  lakini hatuna shaka na namna walivyoitangaza bidhaa yetu, imani yetu kubwa ni kuwa  mkataba huu mpya itakuwa chachu kwao ya kufanya vizuri zaidi msimu ujao”  alisema.

Kwa upande wake Meya wa jiji la Mbeya, alisema kuwa  anaishukuru kampuni hii kwa kuthamini mchango wa City licha ya matokeo mabaya  msimu uliopita.

“Hatukuwa sawa msimu uliopita, matokeo tuliyoyapata si yale ambayo tumekuwa tukiyapata mismu miwili iliyopita, imani yangu kubwa tutafanya vizuri msimu ujao, nawashukufru Binslum kwa kutambua mchango wetu kwao, hii ni chachu kwetu kuelekea mafanikio ya msimu ujao” alisema.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment